MNYAMA AMVUTIA KASI MWARABU KWA MKAPA KIMATAIFA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Wednesday 27 March 2024

MNYAMA AMVUTIA KASI MWARABU KWA MKAPA KIMATAIFA

 


KIKOSI cha Simba kimerejea Dar baada ya kuweka kambi Zanzibar kwa muda ikiwa ni maandalizi ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa.

Ni Machi 29 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa ambapo kwa sasa hamasa zinaendelea mtaa kwa mtaa kuwahamasisha mashabiki wa Simba kujitokeza Uwanja wa Mkapa kushuhudia mchezo huo.

Ahmed Ally, Meneje wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba amesema kuwa Ijumaa kazi ni moja kwa mashabiki kujitokeza uwanjani kushangilia mwanzo mwisho katika mchezo huo na malengo ni kuona wanapata ushindi ndani ya dakika 90.

 

 

KOCHA APEWA MAJUKUMU MAZITO

Ally amesema kuwa uzoefu alionao kocha wa timu hiyo ni moja ya sababu itakayoongeza nguvu kwa timu hiyo kuvuka hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika na kutinga hatua ya nusu fainali.

Ikumbukwe kwamba Simba hesabu kubwa kwa msimu huu ni kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kugotea mara kwa mara hatua ya robo fainali jambo ambalo limewafanya viongozi wa timu hiyo kubainisha kwamba inatosha.

"Kwa uzoefu na ubora wa kocha Abdelhak Benchikha tunaamini atatuvuzusha kwenda Nusu Fainali.

Tunaamini kwamba kila kitu kinawezekana na hilo linatupa nguvu kwa ajili ya kuwa kwenye ushindani mkubwa ambao upo ndani ya uwanja kwa kuwa kila kitu kinawezekana na muda ni sasa.

 “Hakuna katika dunia hii mtu yoyote wakuwazuia mashabiki wa Simba wanapotaka jambo lao, tuungane tupige goti tufanye kila linalowezekana ili tutimize malengo yetu.

“Wachezaji ni wasikivu na wanatambua kazi kubwa inahitajika kufanyika uwanjani hivyo muda ni sasa kuwa kwenye mpango kazi wa kutafuta ushindi ndani ya uwanja, mashabiki tujitokeze kwa wingi kwani kila mchezaji anapenda kuona furaha inabaki ndani ya Simba.

ULINZI KUONGEZEWA DOZI

Benchi la ufundi la Simba limebainisha kuwa makosa ambayo yamekuwa yakifanyika kwenye mechi za ligi yanafanyiwa kazi kwa umakini ili kuwa na safu imara ya ulinzi kwenye mechi zao wanazocheza kutokana na ushindani kuwa mkubwa kitaifa na kimataifa.

Kwenye safu ya ulinzi ni Henock Inonga, Che Malone, Mohmaed Hussein, Shomari Kapombe ni miongoni mwa wachezaji wanaounda safu ya ulinzi ya timu hiyo ya Simba ambayo ina kazi kupambana dhidi ya Al Ahly.

Ipo wazi kwamba ndani ya Ligi Kuu Bara, safu ya ulinzi ya Simba haijawa kwenye mwendo bora katika mechi zake tofauti na zile inazocheza kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Seleman Matola, kocha msaidizi wa Simba amesema kuwa wanatambua makosa yalipo jambo linalowafanya wafanye kazi kwa umakini kuelekea kwenye mechi zijazo kwa kuwaongezea wachezaji wao dozi nyingine.

“Unaona kwenye mechi ambazo tunacheza tunapata ushindi na wakati mwingine tunawapa ruhusa wapinzani kutufunga huwa tunaongea na wachezaji na tutaongeza dozi nyingine kwenye uwanja wa mazoezi.

“Kikubwa ni kuwa makini kwa kuwa mchezo wa mpira ni mchezo wa makosa, kuelekea kwenye mechi zetu zijazo tuna imani tutakuwa imara hilo linawezekana kutokana na wachezaji kujituma na kutimiza majukumu yao kwa ushirikiano,”.

Kikosi cha Simba baada ya kucheza mechi 19 ndani ya ligi ni mabao 18 ukuta umeruhusu ikiwa namba moja kwa timu ambazo zimefungwa mabao mengi ndani ya tatu bora msimu wa 2023/24.

AL AHLY NDANI YA DAR

Kete inayofuata kwa Simba ni Machi 30 2024 itakuwa dhidi ya Al Ahly ambao tayari Machi 27 wameanza mapema safari kwa ajili ya kuwasili Dar kufanya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo.

Mchezo ujao kwa Simba ni wa Ligi ya Mabingwa Afrika itakuwa dhidi ya Al Ahly unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Machi 29 tayari wapinzani wao wameanza safari kuja Dar wanatarajiwa kuwasili Machi 27 kufanya maandalizi ya mwisho kuelekea katika mchezo huo.

Kila timu inautazama mchezo huo kwa hesabu kubwa za kupata ushindi kutokana na ukubwa wa mashindano hayo barani Afrika.

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad