JESHI LA YANGA LITAKALOIBUKA KWA MADIBA HILI HAPA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Tuesday 2 April 2024

JESHI LA YANGA LITAKALOIBUKA KWA MADIBA HILI HAPA

 


MSAFARA wa kikosi cha Yanga umekwea pipa mapema Aprili 2 2024 kuwafuata wapinzani wao Mamelodi Sundowns kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa unaotarajiwa kuchezwa Aprili 5 siku ya Ijumaa.

Ni mchezo wa hatua ya robo fainali ikiwa ni mkondo wa pili baada ya ule uliochezwa Machi 30 ubao wa Uwanja wa Mkapa kusoma Yanga 0-0 Mamelodi Sundowns.

Hiki hapa kikosi cha Yanga chenye wachezaji 26 namna hii:-

Djigui Diarra,
 Aboutwalib Mshery na  Metacha Mnata kwa upande wa makipa ambapo chaguo la kwanza ni Diarra
 Bakari Mwamnyeto, Ibrahim Bacca,  Dickson Job, Yao Attohoula, Nickson Kibabage, Joyce Lomalisa, Gift Fred na Kibwana Shomari upande wa mabeki.

Viungo wa ukabaji ni  Khalid Aucho, Zawadi Mauya, Salum Abubakar, (Sure Boy), Jonas Mkude, Mudathir Yahya na Maxi Nzengeli

Viungo washambuliaji kuna Pacome Zouzoua, Aziz Ki, Augustine Okrah, Skudu Makudubela, Farid Mussa
na Denis Nkane.


Washambuliaji ni Clement Mzize,  Joseph Guede na Kennedy Musonda ambapo kwenye mchezo wa Uwanja wa Mkapa wote walipata nafasi ya kuchez.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad