SIMBA KUJIPANGA UPYA TENA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Sunday, 2 June 2024

SIMBA KUJIPANGA UPYA TENA


 
UONGOZI wa Simba umeweka wazi kuwa utafanyia kazi makosa ambayo yamepita ili kurejea kwenye ubora wao kwa kuwa nyakati ambazo wamepita zimewaumiza.

Ipo wazi kuwa Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Juma Mgunda imegotea nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 69.

Kwenye mchezo wa funga msimu 2023/24 ilikuwa ni dhidi ya Geita Gold waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 watupiaji wakiwa ni Saido Ntibanzokiza na Willy Onana.

Imepishana na taji la ligi pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika na inakwenda kushuhudia bingwa mpya wa CRDB Federation Cup akipatikana leo kati ya Azam FC na Yanga, fainali inayotarajiwa kuchezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba ameweka wazi kuwa nyakati ambazo wamepitia ni ngumu na hazijawafurahisha hivyo wanapambana kurejea kwenye ubora.

“Hatujapenda na tumekuwa na huzuni kwa kuwa tumepoteza kila kitu ambacho tulikuwa tunakipigania kwenye msimu ulioisha.

“Yote kwa yote yaliyopita tunayachukua na tunakwenda kuyafanyia kazi kwa ajili ya kuwa bora wakati ujao mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi.”

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad