BALOZI wa Japan nchini Tanzania Masaharu Yoshida
amefungua rasmi mashindano ya taifa ya mchezo wa baseball na softball
unaozihushisha timu saba za mikoa mbalimbali nchini Tanzania yenye lengo la
kupata timu nzuri ya taifa itakayoshiriki kwenye mashindano ya kimataifa ya
Olimpiki yatakayofanyika Tokyo mwaka 2020
| Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaharu Yoshida (Kulia) |
Akizindua
mashindano hayo Dar es Salaam amesema kuwa anafurahi kuwa miongoni mwa watu
muhimu kaika ufunguzi wa mashindano ya mchezo huo ambao ni maarufu sana nchini
Japan na kuahidi kutoa ushirikiano mzuri ili kuleta maendeleo ya mchezo huo
nchini
“Serikali ya
Japan inaahidi kuwa bega kwa bega katika kuhakikisha kuwa mchezo wa baseball
unapiga hatua na tunaahidi kujenga uwanja wa mazoezi katika shule ya sekondari
ya Azania utakaopewa jina la “Koshien” ambayo ni sehemu ambapo mechi za timu za
shule za ngazi ya juu Japan huwa zinachezwa”alisema.
Aidha
alisema kuwa anapata faraja kuona mashindano ambayo yanawahusisha wachezaji
vijana waliojifunza na kujiandaa wakiwa
wenye morali na nguvu kwa ajili ya kushindana na kuwatakia kila la kheri
katika mashindano.
Katibu Mkuu
wa Chama cha Baseball na Softball Tanzania (TaBSa) Alpherio Nchimbi
alisema kuwa timu zimewasili salama na
mashindano yameshafunguliwa rasmi hivyo na kila kitu kinakwenda sawa na kuwasihi wadau
waweze kujitokeza kuyatazama mashindano hayo yanayowahusu wanafunzi wa
sekondari.
“Mashindano
yameshafunguliwa rasmi ambapo timu saba ndizo zipo kwenye makundi na timu
zilizofungua pazia la mashindano ni Kibasila na Juhudi,ushindani uliopo ni mkali
na hii inaleta hamasa na tunaamini tutapata timu ya taifa yenye ubora ambayo
itaiwakilisha vema Tanzania katika mashindano ya kimataifa “alisema.
Alisema kuwa
mashindano hayo yaliyopewa jina la Uhuru Cup yanaongozwa na kauli mbiu
inayosema Uhuru na kazi kwa kuwa michezo
ni elimu na ajira hivyo amewataka watanzania kuwekeza pia kwenye mchezo wa
Baseball ambao nao ni sehemu ya michezo inayofuatiliwa duniani
Mohamed Pazi
Mwalimu wa Juhudi sekondari amesema kuwa ni wakati wa wazazi na walezi kutumia
fursa hii kwa kuwaruhusu watoto kushiriki kwenye michezo wawapo mashuleni kwa
kuwa michezo ni afya pia ni sehemu inayowakutanisha watu mbalimbali na kuongeza
urafiki na mahusiano baina ya wanamichezo.
“Watoto
wapewe ruhusa kushiriki michezo mbalimbali wakiwa shuleni hata kipindi cha
likizo kwa kuwa hii ni fursa ya kuwapatia watoto ajira na kuwaimarisha kiafya
zaidi kwa mafunzo wanayoyapata wakiwa kambini”,alisema.
Mashindano
hayo yana zihusisha timu kama Azania,Kibasila na Juhudi za Dar Es Salaam,Iyunga
ya Mbeya,Sanya juu ya Kilimanjaro,Mwanakwereke C ya Zanzibar,Kombaini ya
Mwanza,Dodoma yanafanyika katika viwanja vya Azania.
No comments:
Post a Comment