Dr Shule atoa somo kwa wajasiriamali - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Tuesday, 20 December 2016

Dr Shule atoa somo kwa wajasiriamali


WANANCHI wametakiwa kujitokeza katika maonesho la wazi linalojumuuisha makundi yote yaliyo katika sekta ya kilimo ambao ni pamoja na wakulima,wafugaji ,wavuvi na wawindaji yanayotarajiwa kufanyika katika viwanja vya Chuo kikuu cha Dar es Salaam kuanzia desemba 22 hadi 24 mwaka huu.

Dr Vincesia Shule (kulia) akifafanua jambo kuhusu mkulima market
Akizungumza Dar es Dar es Salaam Vincesia Shule Mwandaaji wa maonesho hayo alisema kuwa lengo la kufanya shughuli hiyo ni kuhakikisha wanatoa fursa na upatikanaji wa soko kwa wajasiriamali wadagowadogo na kuwawezesha wananchi kuziona bidhaa zinazozalishwa na wakulima na hakutakuwa na kiingilio.

“Tunatoa fursa kwa wakulima kuweza kupata soko la uhakika na kutafuta suluhu za wajasiriamali katika kuwa wabunifu zaidi ili waweze kujikwamua kwa kupitia bidhaa zao pamoja na kuwapa ujuzi wa namna ya kuzalisha bidhaa zinazoendana na uhitaji pamoja na kupata nembo ya ubora ya TBS kwenye bidhaa zao”alisema


Aidha aliongeza kwa kusema kuwa wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali ili kuweza kuwafikia wakulima na kuwapa taarifa zinazohusu upatikanaji wa masoko na bidhaa kwa wakulima kupitia vyombo vya habari ili kuweza kuimarisha ushindani katika masoko mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad