WASANII
wametakiwa kuwa wabunifu na kushirikiana
katika tasnia ya filamu ili waweze kurudisha soko ambalo limeonekana kuanza
kuyumba .
Katibu wa
chama cha wasanii Mkoani Pwani (TDFAA) Kadnas Nassir alisema kuwa bado wana
nafasi ya kurejesha heshima sokoni.
“Tukiwa
wabunifu zaidi kwa kucheza sinema zenye maadili zinazozungumzia jamii tunauwezo
wa kurudi kwenye ramani na kufanya vizuri hadi ngazi za kimataifa”alisema
Nassir
Alisema kuwa
miongoni mwa sababu zinazoua soko mtandao unaotafsiri filamu za kigeni kwa
kuweka maneno ya kiswahili hali inayodororesha soko na kupoteza mapato kwa
serikali .
“Hawa
wanaotafsiri wanachukua filamu kwenye mtandao ni maharamia kwa kuwa hawalipi
kodi ila kazi tunalipia kodi hivyo mashabiki wathamini vitu vya ndani kwa
manufaa ya taifa”alisema.
No comments:
Post a Comment