MSANII wa
muziki wa kizazi kipya kwa mtindo wa “Hiphop” ametakiwa kutobweteka kutokana na
kuwa gumzo midomoni mwa watu pamoja na nyimbo zake kupigwa kila kona.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti Dar es Salaam
mashabiki wamesema kuwa kwa kukubalika huko yampasa kufanya kweli na kuongeza
juhudi ili abaki kileleni.
Christina Anold ambaye ni mwanamitindo amesema
kuwa afanye mithili ya mashairi yake yanavyosema katika wimbo wake wa maisha na
muziki atazidi kufanya vizuri.
“Amesoma
muziki na kujua mashabiki wanataka nini akisimamia pale anposema kazi juu ya
kazi hatasahulika atazidi kuongeza mashabiki na kuendelea kung’ara kwenye fani
ila asibwete na umaarufu”alisema Christina.
Hassani
Mpate ambaye ni msanii wa filamu alisema kuwa mafanikio ya muda mfupi ayakatae
badala yake aongeze juhudi ili awe wa kimataifa katika fani ya muziki.
“Mashairi
yake mwenyewe yanamfunga kwa mfano anasema usipotembea utabebwa mgongoni akijisahau
tu mashairi yamhukumu na mashabiki watamsahau”alisema Mpate.
Nyimbo tatu
alizoziachia kwa mpigo ambapo kama ingekuwa kwenye mpira ingeitwa “hat trik”
Kama utanipenda na Too much zimepokelewa vema huku ile ya muziki ukiendelea
kubamba mtaani na kuwa kama wimbo wa taifa

No comments:
Post a Comment