WANAFUNZI
wametakiwa kuwekeza nguvu katika masomo yao ili waweze kupata matokeo
yatakayotoa mwanga kwa wazazi na walezi kuwa na moyo wa kuwagharamia zaidi
katika elimu.
Akizungumza
na wanafunzi wa chuo hicho Waziri wa Elimu wa Serikali ya wanafunzi (DASJOSO)
Saitoti Mwalimu alisema kuwa ni jukumu la kila mwanafunzi kuhakikisha kuwa
anasoma pasipo kukata tamaa.
“Lengo kubwa
la mzazi kumpeleka mtoto shule ni kuweza kuona anafikia ndoto zake na kuweza
kuihi maisha anyoyataka na sio yale anayoyaweza hivyo kuna ulazima wa kuongeza
juhudi katika masomo”alisema Mwalimu.

|
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari DSJ wakijiandaa na mitihani inayotarajiwa kuanza hivi karibuni
|
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti na MMG Unique wanafunzi hao,Racheal Kidomo,Patric William,walisema kuwa
ya wanafunzi ni kuhakikisha wanafaulu kwenye masomo pamoja na kuongeza ujuzi
katika fani ya uandishi .
“Kila
mwanafunzi anaishi katika ndoto zake na anaamini kufanya vizuri katika mitihani
pamoja na kufanya kazi kwa vitendo ili kuongeza ujuzi zaidi katika tasnia
inayohitaji ubunifu kila iitwapo leo”alisema Kidomo.
Patric Wiliam ambaye ni mwanafunzi wa ngazi ya
stashada alisema kuwa matokeo mabaya
yanaumiza kwani hakuna anayepanda akitarajia mavuno haba hivyo kuna umuhimu wa kila mwanafunzi
kuzingatia kile anachojifunza na kufanyia kazi.
No comments:
Post a Comment