Na .Victor Denis
Dar es Salaam
JAMII imetakiwa kutumia mitandao ya kijamii kwa kujitangaza hasa
ili kuweza kufanya vema katika ushindani wa kibiashara hali itakayoweza kuwapa
mafanikio katika kazi zao..
Akizungumza na wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam wakala wa
Google Tanzania Angel Ernest alisema kuwa hakuna kinachoshindikana katika
ulimwengu
wa teknolojia ya habari.
“Kuna maana kubwa sana katika matumizi ya kuwa makini katika
mitandao ya kijamii uwezo wa wale ambao wanaweza kugharamia masuala kazi za
kwenye mitandao wana nafasi ya kufanya vizuri hasa kwenye ushindani na
kujipatia kipato “alisema
Aidha aliwataka wanafunzi kuweza kuwa na tabia ya kuwa wepesi
katika kuhakikisha kuwa wanatuma habari ambazo zinaishi tofauti na kuishia kutuma
picha za kawaida ambazo hazina manaufaa kwa mtu yeyote zaidi ya kujifurahisha
tu “ alisema
Zainab Mbaraka ambaye ni Katibu Mkuu Serikali ya Wanafunzi
DASJOSO alisema kuwa wamenufaika na semina hiyo kwani imeweza kuwapa mwanga
katika hali ya kuwa katika uwezo mpya hasa kwa matumizi ya mitandao ya kijamii.

No comments:
Post a Comment