CEDRICK Kaze aliyekuwa kocha msaidizi kwenye kikosi cha Yanga yenye maskani yake mitaa ya Kariakoo kwa sasa atakuwa Kocha Mkuu Namungo FC.
Kaze alipewa mkono wa asante ndani ya Yanga baada ya msimu wa 2022/23 kugota mwisho.
Anaibukia ndani ya Namungo FC inayoshiriki Ligi Kuu Bara hivyo atakuwa na nafasi ya kukutana na waajiri wake wa zamani kwenye mechi za ushindani.
Ndani ya Namungo ambapo ametambulishwa Julai 24 atashirikiana na Dennis Kitambi na Shadrack Nsajigwa kukiongoza kikosi cha Namungo.
No comments:
Post a Comment