Dizo Click

Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Post Top Ad

Sunday, 23 November 2025

CAF Champions League: Simba SC 0-1 Petro de Luanda

22:38 0


CAF Champions League

Uwanja wa Mkapa

FT: Simba SC 0-1 Petro de Luanda

Novemba 23,2025

 Bernardo Dias dakika ya 78. Pasi ya goli hilo pekee la ushindi imetoka kwa Tiago Reis.

 Kipindi cha pili 

Dakika ya 90 Jean Ahoua anaonyeshwa kadi ya njano

Dakika ya 84 Kante out in Mukwala

Dakika ya 78 Goal kwa Petro de Luanda, Benrnardo

Dakika ya 74 Ladack Chasambi of target 

Dakika ya 72 Ladack Chasambi anaingia anatoka Abrahm Morice 

Dakika ya 65 Sowah anachezewa faulo

Dakika ya 64 Yakoub anaokoa hatari

Mpanzu cheza faulo dk 55

Ahoua in out Camara dk 53

Sowah in out Mutale dk 53

Mpanzu mis chance dk 52

Dakika ya 50 Rushine cheza faulo ndani ya 18

Dakika ya 46 Nangu piga faulo

Dakika 2 zimeongezwa kipindi cha pili

Dakika ya 45 Nangu anaokoa hatari

Dakika ya 37 Mutale cheza faulo

Dakika ya 34 De Reuck anapiga faulo 

Dakika ya 32 De Reuck of target 

Dakika ya 22 Morice anakosa nafasi ya wazi ndani ya 18 kwa pasi ya Shomari Kapombe 

Dakika ya 20 jezi namba 24 njano kwa kumchezea faulo Mpanzu

Dakika ya 17 Morice oftarget 

Dakika ya 16 Mutale chezewa faulo

Dakika ya 13 Mpanzu of target 

Dakika ya 7 Mutale ofside 

Dakika ya kwanza Mutale anzisha mpira

Read More

Saturday, 22 November 2025

YANGA SC 1-0 AS FAR RABAT LIGI YA MABINGWA AFRIKA, DUBE AFUNGA

18:20 0

 


CAF Champions League ubao wa Uwanja wa New Amaan Complex umesoma Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat mchezo wa hatua ya makundi Jumamosi ya Novemba 22,2025.


Goli la ushindi limefungwa na mshambuliaji Prince Dube ambaye alianza kikosi cha kwanza. Ni dakika ya 58 Dube alipachika bao hilo kwa pasi ya kiungo Mudathir Yahya.

Kampeni za hatua ya robo fainali zimeanza huku Yanga SC kete ya kwanza wakikomba pointi tatu kundi B.

Msimamo kundi B huu hapa

1. Yanga SC pointi 3 mechi 1
2. JS Kabylie pointi 0 mechi 0
3. Al Ahly pointi 0 mechi 0
4. AS FAR Rabat pointi 0 mechi 1

Yanga SC chini ya Kocha Mkuu, Pedro imeanza kwa ushindi ikiwa ni mchezo wa kwanza wakiwa nyumbani katika hatua ya makundi.

Read More

Sunday, 26 October 2025

Simba SC vs Nsingizini kitaumana

07:16 0

 


Simba SC vs Nsingizini Hotspurs CAF Champions, kitaumana kwa Mkapa kwa wababe hawa Oktba 26 kila timu kusaka tiketi ya kutinga hatua ya makundi.

Ikumbukwe kwamba katika mchezo wa kwanza ugenini Oktoba 19,2025 ilikuwa Nsingizini Hotspurs 0-3 Simba SC. Mchezo wa maamuzi utapigwa Uwanja wa Mkapa kwa wababe hawa wawili kusaka timu itakayokwenda hatua ya makundi.

Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa huo ni mchezo wa kazi na watapambana kupata matokeo mazuri uwanjani.

“Kikosi Jumatano  kinarudi Mo Simba Arena kuanza maandalizi ya mchezo wa Jumapili. Tunayo furaha ya kocha wetu Seleman Matola amemaliza adhabu yake hivyo atakuwepo kwenye benchi Jumapili kuendelea na majukumu yake.

“Kuelekea mchezo huu tumeweka viingilio vya kitajiri. Viingilio ni Tanzanite - Tsh. 250,000, Platinum - Tsh. 150,000, VIP A - Tsh. 30,000, VIP B - Tsh. 20,000, VIP C - Tsh. 10,000 na Mzunguko - Tsh. 5,000.

“Afrika hii timu zenye uhakika wa kucheza makundi mara saba mfululizo ni Al Ahly na Mamelodi na sisi tunaongezeka hapo. Ni mechi ambayo inatuongezea thamani kwenye klabu yetu. Na Mwanasimba asitokee akaidharau hii mechi, tuutizame huu mchezo kama mchezo mpya. Itakuwa haina maana yoyote tuje hapa tufungwe bao moja au mbili au twende matuta hatupo tayari kuona hiyo fedheha. Tuhesabu bado ni bilabila.

“Mpaka sasa sisi tumeshinda mechi moja na bado hatujafuzu. Mechi hii ya kufuzu tunataka kujaza uwanja wa Mkapa, hatutakiwi kuchukulia poa, kwenye mpira hakuna kitu cha kawaida. Twendeni tukaujaze Uwanja wa Benjamini Mkapa. Na sare yetu siku ya Jumapili itakuwa ni jezi nyekundu ya kuscan. Usije na jezi ya zamani tafadhali, kila Mwanasimba aje na jezi mpya ya Jayrutty.

“Wanasimba tunasababu za kuja uwanjani maana mechi iliyopita tuliangalizia mchezo tukiwa Coco Beach, ilituuma. Tunalazimika kwenda uwanjani ili kumkaribisha Meneja Dimitar Pantev akutane na Wanasimba kwa mara ya kwanza, aione Simba Sports Club ipoje. Kwa kifupi Oktoba 26 itakuwa Simba Day ya Pantev maana ile nyingine hakuwepo," Semaji Ahmed Ally.

 

Read More

Wednesday, 22 October 2025

Yanga SC vs Silver Strikers Jumamosi hakuna kiingilio

10:10 0

 


CAF Champions League, Oktoba 25 2025 uongozi wa Yanga SC umeweka wazi kuwa mechi hiyo itakuwa mikononi mwa mashabiki hivyo wajitokeze kwa wakati kuishangilia timu hiyo na kuipeleka hatua ya makundi.

Hiyo imetokana na mashabiki wengi kufunga safari kuelekea nchini Malawi kuishangilia timu hiyo Oktoba 18, 2025 kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Bingu matokeo yaliposoma Silver Strikers 1-0 Yanga SC.

Yanga SC inahitaji ushindi wa angalau goli 2-0 katika mchezo wa Oktoba 25,2025, Uwanja wa Mkapa huku mashabiki wakiombwa kuwa wastaarabu na wasifanye vurugu yoyote ile wala kuwasha moto wakiwa uwanjani.

Ali Kamwe Ofisa Habari wa Yanga SC amesema kuwa wanachama wa Yanga SC waliomba mechi ya Jumamosi kusiwe na viingilio jambo ambalo limefanyiwa kazi na uongozi kwa umakini mkubwa na kuamua iwe hivyo.

“Tumepokea maoni mengi kutoka kwa Wanachama wetu wakiuomba uongozi wa Yanga kuwa mechi ya jumamosi usiwe na viingilio, tuwaachie wao mchezo huu na tuwape nafasi ya wao kuisapoti timu yetu na kuivusha kwenda hatua ya makundi.

“Tayari uongozi wetu umekutana na kujadili maoni haya ya wanachama na kimsingi wamelipokea, wamekubaliana na kulipitisha ombi hili la Wanachama wetu. Hivyo ombi limekubaliwa na mashabiki wawe makini kwenye mchezo wetu wasilete vurugu.

“Ikitokea ni shabiki wa Mtibwa Sugar, Mbeya City ama timu yoyote amekuja usimsumbue muache aangalie mpira apate burudani lakini akija a malengo tofauti huyo lazima aondolewe kwa kuonyeshwa mlango wa kutokea,”  Ally Kamwe

Read More

Monday, 20 October 2025

Simba SC vs Nsingizini Hotspurs , Kibu Dennis kwenye kazi nyingine

09:16 0


AHMED Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa bado hawajatinga hatua ya makundi kutokana na ugumu wa kila mchezo CAF Champions League.

Simba SC Oktoba 19,2025 ilipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Nsingizini Hotspurs uliochezwa Uwanja wa Somholo, mchezo wa pili unatarajiwa kuchezwa Oktoba 26,2025 Uwanja wa Mkapa.

“Tumepata ushindi wa mabao 3-0 ugenini haya matokeo ni zawadi kwa mashabiki wa Eswatini, hawa Nsingizni sio timu ya kubeza hata kidogo kazi haijaisha,”.

Mchezo huo ulichezwa Uwanja wa Somhlolo, nchini Eswatini ulikuwa na ushindani mkubwa. Kipindi cha kwanza timu zote mbili zilishambuliana kwa zamu, huku Simba SC wakifanikiwa kutengeneza nafasi nyingi zaidi. Bao la kwanza la mchezo huo lilikuja dakika ya 45 ya mchezo, kupitia kwa mlinzio wa Simba SC, Wilson Nangu.

Nangu alifunga bao hilo la kuongoza kwa kuunganisha kwa kichwa krosi nzuri ya kona ya kiungo, Neo Maema. Mara tu, baada ya bao hilo kipyenga cha mwamuzi kikasikika na timu Kwenda mapumziko.

Kibu Dennis ambaye aliingia kipindi cha pili alifunga maao mawili dakika ya 82 na 89 amebainisha kuwa bado wana kazi nyingine kuelekea mchezo wa marudiano Uwanja wa Mkapa.

Read More

Saturday, 18 October 2025

Yanga SC yaachana na Romain Folz mazima

22:52 0


RASMI uongozi wa Yanga SC Oktoba 18,2025 umetoa taarifa ya kuachana na Romain Folz ambaye alikuwa kocha mkuu wa timu hiyo.

Mchezo wa mwisho kukaa benchi ni Oktba 18,2025 ubao wa Uwanja wa Bingu umesoma Silver Strikers 1-0 Yanga SC, CAF Champions League.

Taarifa kutoka Yanga SC imeeleza namna hii:-“Uongozi wa Young African Sports Club unapenda kuutarifu Umma kuwa, umevunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza, Romain Folz.

“Uongozi wa Young African Sports Club unamshukuru kocha Romain Folz kwa mchango wake ndani ya klabu yetu na unamtakia kila la kheri katika majukumu yake yanayofata.

“Katika kipindi hiki kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha msaidizi Patrick Mabedi huku mchakato wa kutafuta kocha mkuu ukiendelea,” .

Read More

Friday, 17 October 2025

Kamata ratiba ya mechi za kimataifa na muda utakaochezwa

08:35 0


WAWAKILISHI wa Tanzania watakuwa kazini kwenye mechi za kimataifa ikiwa ni katika Kombe la Shirikisho Afrika na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Tanzania inawakilishwa na nchi nne ambazo ni Simba SC na Yanga SC katika Ligi ya Mabingwa Afrika na Azam FC dhidi ya Singida Black Stars.  

Ni Jumamosi, Yanga SC watakuwa Uwanja wa Bingu nchini Malawi wakicheza na Silver Striker, kuwania kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki na itarushwa mubashara kupitia AzamSports2HD.

Jumapili, Simba SC watakuwa Eswatini katika Uwanja wa Somhlolo wakicheza na Nsingizini Hotspurs kuwania kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:00 jioni na kuruka mubashara kupitia AzamSports2HD.


Kwa Kombe la Shirikisho Afrika ipo namna hii:-

Jumamosi, KMKM watakuwa nyumbani Uwanja wa Amaan wakiwakaribisha matajiri wa Chamazi, Azam FC.

Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:15 jioni na kuruka mubashara kupitia AzamSports4HD.


Jumapili, Singida BS watakuwa jijini Bunjumbura katika Uwanja wa Prince Louis Rwagasore wakicheza na Flambeau Du Centre.

Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:00 jioni, na itakuwa mubashara kupitia AzamSports4HD.



Read More

Post Top Ad