Post Top Ad
Post Top Ad
Saturday, 9 August 2025
Friday, 11 July 2025
BEKI MPYA SINGIDA BLACK STARS AFUNGUKA
NYOTA Kelvin Kijili ambaye ni ingizo jipya ndani ya Singida Black Stars akitokea kikosi cha Simba SC ameweka wazi kuwa yupo tayari kwa ajili ya kupambana kutimiza majukumu kwenye timu hiyo kitaifa na kimataifa.
Kijili ametambulishwa rasmi ndani ya Singida Black Stars Julai 10 2025 ikiwa ni mchezaji wa kwanza kutambulishwa ndani ya Singida Black Stars.
Msimu wa 2024/25 alikuwa ndani ya kikosi cha Simba SC. Kwenye kikosi cha Simba SC hakuwa na nafasi kikosi cha kwanza hakufikisha mechi 15 za ligi kati ya 30 ambazo timu hiyo ilicheza.
Anajiunga na Singida Black Stars ambayo itashiriki Kombe la Shirikisho Afrika chini ya Kocha Mkuu, Miguel Gamondi ambaye aliwahi kuifundisha Yanga SC.
Kijili amesema: "Nimefurahi kusaini mkataba ndani ya Singida Black Stars nina amini kwamba nitafanya kazi kubwa kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu kitaifa na kimataifa."
Ni miaka miwili amesaini mchezaji huyo kwa ajili ya changamoto mpya msimu wa 2025/26 amerejea nyumbani kwa mara nyingine tena.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.
CLATOUS CHAMA KWENYE RADA ZA ZESCO UNITED
KIUNGO mshambuliaji wa Yanga SC, Clatous Chama anatajwa kuwa kwenye rada za Klabu ya Zesco United ya Zambia.
Chama ambaye alitambulishwa rasmi Yanga SC Julai Mosi 2024, mkataba wake wa mwaka mmoja umeggota mwisho.
Alitambulishwa hapo akiwa mchezaji huru akitokea kikosi cha Simba SC ambacho kimegotea nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
Taarifa zinaeleza kuwa mazungumzo ya wakala wa Chama na Zesco United yamefikia kwenye hatua nzuri kilichobaki nyota huyo kusaini na kutambulishwa ikiwa mabosi wa Yanga SC watamchunia moja kwa moja.
Yanga SC wanatambua mkataba wa mchezaji huyo umeisha na hawajafanya mazungumzo yoyote jambo linaloashiria kwamba ni asilimia kubwa hatakuwa kwenye ligi namba nne kwa ubora Afrika Clatous Chama msimu wa 2025/26.
Msimu wa 2024/25, Chama alifunga mabao sita na katika mabao hayo mabao mawili alifunga kwa mapigo huru akiwa nje ya 18.
Imeandikwa
na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo,
kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya
Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa
Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa
Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo
Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.
Sunday, 20 April 2025
FOUNTAIN GATE WAZITAKA POINTI TATU ZA YANGA
WAPINZANI wa Yanga ndani ya Ligi Kuu Bara kuelekea kwenye mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa Aprili 21 2025 Uwanja wa Tanzanite, Kwaraa Fountain Gate wamebainisha kuwa wamepata mbinu za wapinzani wao hivyo wanajua namna watakavyofanya kazi kuwadhibiti.
Yanga ni vinara ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mechi 25 ni pointi 67 wamekusanya kibindoni na safu ya ushambuliaji imetupia jumla ya mabao 64 ikiwa ni safu kali kwenye kumalizia nafasi ambazo zinatengenezwa ndani ya uwanja kwenye ligi.
Inakutana na Fountain Gate ambayo namba mbili kwa timu ambazo zimeruhusu mabao mengi ndani ya ligi ambayo ni 47 baada yakucheza mechi 26 ikiwa nafasi ya 9 na pointi zake kibindoni ni 29.
Issa Mbuzi amesema kuwa wanatambua ubora wa Yanga ulipo na udhaifu kwa kuwa waliwatazama kwa ukaribu kwenye mchezo dhidi ya Stand United uliochezwa Uwanja wa KMC, Complex, Aprili 15 2025 na ubao ukasoma Yanga 8-1 Stand United.
“Tunawatambua vizuri hawa Yanga na kwenye mchezo wao dhidi ya Stand tulikuwa na wataalamu wakusoma mbinu zaidi ya wanne, wameniambia wameona namna itakayotupa matokeo kwenye mchezo wetu Aprili 21 tukiwa nyumbani.
“Eneo la kiungo kuna matatizo pale na wanaye Aziz Ki ambaye huyu tutampa mtu wakutembea naye hatua kwa hatua ndani ya uwanja, utakuwa mchezo mgumu lakini tunahitaji pointi tatu zao ili tujihakikishie nafasi ya sita kwenye msimamo.”
Imeandikwa na
Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata
TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika,
usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa
Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa
unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja
Damu usipange kukosa.
Sunday, 2 June 2024
SIMBA KUJIPANGA UPYA TENA
UONGOZI wa Simba umeweka wazi kuwa utafanyia kazi makosa ambayo yamepita ili kurejea kwenye ubora wao kwa kuwa nyakati ambazo wamepita zimewaumiza.
Ipo wazi kuwa Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Juma Mgunda imegotea nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 69.
Kwenye mchezo wa funga msimu 2023/24 ilikuwa ni dhidi ya Geita Gold waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 watupiaji wakiwa ni Saido Ntibanzokiza na Willy Onana.
Imepishana
na taji la ligi pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika na inakwenda kushuhudia
bingwa mpya wa CRDB Federation Cup akipatikana leo kati ya Azam FC na Yanga,
fainali inayotarajiwa kuchezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Ahmed Ally,
Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba ameweka wazi kuwa nyakati ambazo
wamepitia ni ngumu na hazijawafurahisha hivyo wanapambana kurejea kwenye ubora.
“Hatujapenda na tumekuwa na huzuni kwa kuwa tumepoteza kila kitu ambacho tulikuwa
tunakipigania kwenye msimu ulioisha.
“Yote kwa
yote yaliyopita tunayachukua na tunakwenda kuyafanyia kazi kwa ajili ya kuwa
bora wakati ujao mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi.”
Tuesday, 2 April 2024
JESHI LA YANGA LITAKALOIBUKA KWA MADIBA HILI HAPA
MSAFARA wa kikosi cha Yanga umekwea pipa mapema Aprili 2 2024 kuwafuata wapinzani wao Mamelodi Sundowns kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa unaotarajiwa kuchezwa Aprili 5 siku ya Ijumaa.
Ni mchezo wa hatua ya robo fainali ikiwa ni mkondo wa pili baada ya ule uliochezwa Machi 30 ubao wa Uwanja wa Mkapa kusoma Yanga 0-0 Mamelodi Sundowns.
Hiki hapa kikosi cha Yanga chenye wachezaji 26 namna hii:-
Djigui
Diarra, Aboutwalib Mshery na Metacha
Mnata kwa upande wa makipa ambapo chaguo la kwanza ni Diarra
Bakari
Mwamnyeto, Ibrahim
Bacca, Dickson
Job, Yao
Attohoula, Nickson
Kibabage, Joyce
Lomalisa, Gift
Fred na Kibwana
Shomari upande wa mabeki.
Viungo wa ukabaji ni Khalid
Aucho, Zawadi
Mauya, Salum
Abubakar, (Sure Boy), Jonas
Mkude, Mudathir Yahya na Maxi
Nzengeli
Viungo washambuliaji kuna Pacome Zouzoua, Aziz Ki, Augustine Okrah, Skudu Makudubela, Farid
Mussa
na Denis
Nkane.
Washambuliaji ni Clement
Mzize, Joseph
Guede na Kennedy
Musonda ambapo kwenye mchezo wa Uwanja wa Mkapa wote walipata nafasi ya kuchez.
Wednesday, 27 March 2024
MNYAMA AMVUTIA KASI MWARABU KWA MKAPA KIMATAIFA
KIKOSI cha Simba kimerejea Dar baada ya kuweka kambi Zanzibar kwa muda ikiwa ni maandalizi ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa.
Ni Machi 29 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa
ambapo kwa sasa hamasa zinaendelea mtaa kwa mtaa kuwahamasisha mashabiki wa
Simba kujitokeza Uwanja wa Mkapa kushuhudia mchezo huo.
Ahmed Ally, Meneje wa Idara ya Habari na
Mawasiliano Simba amesema kuwa Ijumaa kazi ni moja kwa mashabiki kujitokeza
uwanjani kushangilia mwanzo mwisho katika mchezo huo na malengo ni kuona
wanapata ushindi ndani ya dakika 90.
KOCHA APEWA MAJUKUMU MAZITO
Ally amesema kuwa uzoefu alionao kocha wa
timu hiyo ni moja ya sababu itakayoongeza nguvu kwa timu hiyo kuvuka hatua ya
robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika na kutinga hatua ya nusu fainali.
Ikumbukwe kwamba Simba hesabu kubwa kwa msimu
huu ni kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kugotea mara kwa mara hatua ya
robo fainali jambo ambalo limewafanya viongozi wa timu hiyo kubainisha kwamba
inatosha.
"Kwa uzoefu na ubora wa kocha Abdelhak
Benchikha tunaamini atatuvuzusha kwenda Nusu Fainali.
Tunaamini kwamba kila kitu kinawezekana na hilo
linatupa nguvu kwa ajili ya kuwa kwenye ushindani mkubwa ambao upo ndani ya
uwanja kwa kuwa kila kitu kinawezekana na muda ni sasa.
“Hakuna
katika dunia hii mtu yoyote wakuwazuia mashabiki wa Simba wanapotaka jambo lao,
tuungane tupige goti tufanye kila linalowezekana ili tutimize malengo yetu.
“Wachezaji ni wasikivu na wanatambua kazi kubwa
inahitajika kufanyika uwanjani hivyo muda ni sasa kuwa kwenye mpango kazi wa
kutafuta ushindi ndani ya uwanja, mashabiki tujitokeze kwa wingi kwani kila
mchezaji anapenda kuona furaha inabaki ndani ya Simba.
ULINZI KUONGEZEWA DOZI
Benchi la ufundi la Simba limebainisha kuwa
makosa ambayo yamekuwa yakifanyika kwenye mechi za ligi yanafanyiwa kazi kwa
umakini ili kuwa na safu imara ya ulinzi kwenye mechi zao wanazocheza kutokana
na ushindani kuwa mkubwa kitaifa na kimataifa.
Kwenye safu ya ulinzi ni Henock Inonga, Che
Malone, Mohmaed Hussein, Shomari Kapombe ni miongoni mwa wachezaji wanaounda
safu ya ulinzi ya timu hiyo ya Simba ambayo ina kazi kupambana dhidi ya Al
Ahly.
Ipo wazi kwamba ndani ya Ligi Kuu Bara, safu
ya ulinzi ya Simba haijawa kwenye mwendo bora katika mechi zake tofauti na zile
inazocheza kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Seleman Matola, kocha msaidizi wa Simba
amesema kuwa wanatambua makosa yalipo jambo linalowafanya wafanye kazi kwa
umakini kuelekea kwenye mechi zijazo kwa kuwaongezea wachezaji wao dozi
nyingine.
“Unaona kwenye mechi ambazo tunacheza
tunapata ushindi na wakati mwingine tunawapa ruhusa wapinzani kutufunga huwa
tunaongea na wachezaji na tutaongeza dozi nyingine kwenye uwanja wa mazoezi.
“Kikubwa ni kuwa makini kwa kuwa mchezo wa
mpira ni mchezo wa makosa, kuelekea kwenye mechi zetu zijazo tuna imani
tutakuwa imara hilo linawezekana kutokana na wachezaji kujituma na kutimiza
majukumu yao kwa ushirikiano,”.
Kikosi cha Simba baada ya kucheza mechi 19
ndani ya ligi ni mabao 18 ukuta umeruhusu ikiwa namba moja kwa timu ambazo
zimefungwa mabao mengi ndani ya tatu bora msimu wa 2023/24.
AL AHLY NDANI YA DAR
Kete inayofuata kwa Simba ni Machi 30 2024
itakuwa dhidi ya Al Ahly ambao tayari Machi 27 wameanza mapema safari kwa ajili
ya kuwasili Dar kufanya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo.
Mchezo ujao kwa Simba ni wa Ligi ya Mabingwa
Afrika itakuwa dhidi ya Al Ahly unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Machi 29
tayari wapinzani wao wameanza safari kuja Dar wanatarajiwa kuwasili Machi 27
kufanya maandalizi ya mwisho kuelekea katika mchezo huo.
Kila timu inautazama mchezo huo kwa hesabu
kubwa za kupata ushindi kutokana na ukubwa wa mashindano hayo barani Afrika.