Dizo Click

Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Post Top Ad

Sunday, 26 October 2025

Simba SC vs Nsingizini kitaumana

07:16 0

 


Simba SC vs Nsingizini Hotspurs CAF Champions, kitaumana kwa Mkapa kwa wababe hawa Oktba 26 kila timu kusaka tiketi ya kutinga hatua ya makundi.

Ikumbukwe kwamba katika mchezo wa kwanza ugenini Oktoba 19,2025 ilikuwa Nsingizini Hotspurs 0-3 Simba SC. Mchezo wa maamuzi utapigwa Uwanja wa Mkapa kwa wababe hawa wawili kusaka timu itakayokwenda hatua ya makundi.

Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa huo ni mchezo wa kazi na watapambana kupata matokeo mazuri uwanjani.

“Kikosi Jumatano  kinarudi Mo Simba Arena kuanza maandalizi ya mchezo wa Jumapili. Tunayo furaha ya kocha wetu Seleman Matola amemaliza adhabu yake hivyo atakuwepo kwenye benchi Jumapili kuendelea na majukumu yake.

“Kuelekea mchezo huu tumeweka viingilio vya kitajiri. Viingilio ni Tanzanite - Tsh. 250,000, Platinum - Tsh. 150,000, VIP A - Tsh. 30,000, VIP B - Tsh. 20,000, VIP C - Tsh. 10,000 na Mzunguko - Tsh. 5,000.

“Afrika hii timu zenye uhakika wa kucheza makundi mara saba mfululizo ni Al Ahly na Mamelodi na sisi tunaongezeka hapo. Ni mechi ambayo inatuongezea thamani kwenye klabu yetu. Na Mwanasimba asitokee akaidharau hii mechi, tuutizame huu mchezo kama mchezo mpya. Itakuwa haina maana yoyote tuje hapa tufungwe bao moja au mbili au twende matuta hatupo tayari kuona hiyo fedheha. Tuhesabu bado ni bilabila.

“Mpaka sasa sisi tumeshinda mechi moja na bado hatujafuzu. Mechi hii ya kufuzu tunataka kujaza uwanja wa Mkapa, hatutakiwi kuchukulia poa, kwenye mpira hakuna kitu cha kawaida. Twendeni tukaujaze Uwanja wa Benjamini Mkapa. Na sare yetu siku ya Jumapili itakuwa ni jezi nyekundu ya kuscan. Usije na jezi ya zamani tafadhali, kila Mwanasimba aje na jezi mpya ya Jayrutty.

“Wanasimba tunasababu za kuja uwanjani maana mechi iliyopita tuliangalizia mchezo tukiwa Coco Beach, ilituuma. Tunalazimika kwenda uwanjani ili kumkaribisha Meneja Dimitar Pantev akutane na Wanasimba kwa mara ya kwanza, aione Simba Sports Club ipoje. Kwa kifupi Oktoba 26 itakuwa Simba Day ya Pantev maana ile nyingine hakuwepo," Semaji Ahmed Ally.

 

Read More

Wednesday, 22 October 2025

Yanga SC vs Silver Strikers Jumamosi hakuna kiingilio

10:10 0

 


CAF Champions League, Oktoba 25 2025 uongozi wa Yanga SC umeweka wazi kuwa mechi hiyo itakuwa mikononi mwa mashabiki hivyo wajitokeze kwa wakati kuishangilia timu hiyo na kuipeleka hatua ya makundi.

Hiyo imetokana na mashabiki wengi kufunga safari kuelekea nchini Malawi kuishangilia timu hiyo Oktoba 18, 2025 kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Bingu matokeo yaliposoma Silver Strikers 1-0 Yanga SC.

Yanga SC inahitaji ushindi wa angalau goli 2-0 katika mchezo wa Oktoba 25,2025, Uwanja wa Mkapa huku mashabiki wakiombwa kuwa wastaarabu na wasifanye vurugu yoyote ile wala kuwasha moto wakiwa uwanjani.

Ali Kamwe Ofisa Habari wa Yanga SC amesema kuwa wanachama wa Yanga SC waliomba mechi ya Jumamosi kusiwe na viingilio jambo ambalo limefanyiwa kazi na uongozi kwa umakini mkubwa na kuamua iwe hivyo.

“Tumepokea maoni mengi kutoka kwa Wanachama wetu wakiuomba uongozi wa Yanga kuwa mechi ya jumamosi usiwe na viingilio, tuwaachie wao mchezo huu na tuwape nafasi ya wao kuisapoti timu yetu na kuivusha kwenda hatua ya makundi.

“Tayari uongozi wetu umekutana na kujadili maoni haya ya wanachama na kimsingi wamelipokea, wamekubaliana na kulipitisha ombi hili la Wanachama wetu. Hivyo ombi limekubaliwa na mashabiki wawe makini kwenye mchezo wetu wasilete vurugu.

“Ikitokea ni shabiki wa Mtibwa Sugar, Mbeya City ama timu yoyote amekuja usimsumbue muache aangalie mpira apate burudani lakini akija a malengo tofauti huyo lazima aondolewe kwa kuonyeshwa mlango wa kutokea,”  Ally Kamwe

Read More

Monday, 20 October 2025

Simba SC vs Nsingizini Hotspurs , Kibu Dennis kwenye kazi nyingine

09:16 0


AHMED Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa bado hawajatinga hatua ya makundi kutokana na ugumu wa kila mchezo CAF Champions League.

Simba SC Oktoba 19,2025 ilipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Nsingizini Hotspurs uliochezwa Uwanja wa Somholo, mchezo wa pili unatarajiwa kuchezwa Oktoba 26,2025 Uwanja wa Mkapa.

“Tumepata ushindi wa mabao 3-0 ugenini haya matokeo ni zawadi kwa mashabiki wa Eswatini, hawa Nsingizni sio timu ya kubeza hata kidogo kazi haijaisha,”.

Mchezo huo ulichezwa Uwanja wa Somhlolo, nchini Eswatini ulikuwa na ushindani mkubwa. Kipindi cha kwanza timu zote mbili zilishambuliana kwa zamu, huku Simba SC wakifanikiwa kutengeneza nafasi nyingi zaidi. Bao la kwanza la mchezo huo lilikuja dakika ya 45 ya mchezo, kupitia kwa mlinzio wa Simba SC, Wilson Nangu.

Nangu alifunga bao hilo la kuongoza kwa kuunganisha kwa kichwa krosi nzuri ya kona ya kiungo, Neo Maema. Mara tu, baada ya bao hilo kipyenga cha mwamuzi kikasikika na timu Kwenda mapumziko.

Kibu Dennis ambaye aliingia kipindi cha pili alifunga maao mawili dakika ya 82 na 89 amebainisha kuwa bado wana kazi nyingine kuelekea mchezo wa marudiano Uwanja wa Mkapa.

Read More

Saturday, 18 October 2025

Yanga SC yaachana na Romain Folz mazima

22:52 0


RASMI uongozi wa Yanga SC Oktoba 18,2025 umetoa taarifa ya kuachana na Romain Folz ambaye alikuwa kocha mkuu wa timu hiyo.

Mchezo wa mwisho kukaa benchi ni Oktba 18,2025 ubao wa Uwanja wa Bingu umesoma Silver Strikers 1-0 Yanga SC, CAF Champions League.

Taarifa kutoka Yanga SC imeeleza namna hii:-“Uongozi wa Young African Sports Club unapenda kuutarifu Umma kuwa, umevunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza, Romain Folz.

“Uongozi wa Young African Sports Club unamshukuru kocha Romain Folz kwa mchango wake ndani ya klabu yetu na unamtakia kila la kheri katika majukumu yake yanayofata.

“Katika kipindi hiki kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha msaidizi Patrick Mabedi huku mchakato wa kutafuta kocha mkuu ukiendelea,” .

Read More

Friday, 17 October 2025

Kamata ratiba ya mechi za kimataifa na muda utakaochezwa

08:35 0


WAWAKILISHI wa Tanzania watakuwa kazini kwenye mechi za kimataifa ikiwa ni katika Kombe la Shirikisho Afrika na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Tanzania inawakilishwa na nchi nne ambazo ni Simba SC na Yanga SC katika Ligi ya Mabingwa Afrika na Azam FC dhidi ya Singida Black Stars.  

Ni Jumamosi, Yanga SC watakuwa Uwanja wa Bingu nchini Malawi wakicheza na Silver Striker, kuwania kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki na itarushwa mubashara kupitia AzamSports2HD.

Jumapili, Simba SC watakuwa Eswatini katika Uwanja wa Somhlolo wakicheza na Nsingizini Hotspurs kuwania kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:00 jioni na kuruka mubashara kupitia AzamSports2HD.


Kwa Kombe la Shirikisho Afrika ipo namna hii:-

Jumamosi, KMKM watakuwa nyumbani Uwanja wa Amaan wakiwakaribisha matajiri wa Chamazi, Azam FC.

Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:15 jioni na kuruka mubashara kupitia AzamSports4HD.


Jumapili, Singida BS watakuwa jijini Bunjumbura katika Uwanja wa Prince Louis Rwagasore wakicheza na Flambeau Du Centre.

Mechi hii itachezwa kuanzia saa 10:00 jioni, na itakuwa mubashara kupitia AzamSports4HD.



Read More

Friday, 3 October 2025

Simba SC 3-0 Namungo FC, Oktoba 1 2025

14:36 0


 Simba SC 3-0 Namungo FC

Oktoba Mosi 2025

Simba SC imekusanya pointi tatu kwenye mchezo dhidi ya Namungo FC Uwanja wa Mkapa. Beki Rushine alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo.

Zimeongezwa dakika 3

Dakika 90 zimekamilika 

Dakika ya 88 jezi namba 30 piga kona kwa Namungo

Dakika ya 84 Mwalimu goal shoto ndani ya 18

Dakika ya 83 jezi namba 5 njano kwa Simba 

Dakika ya 79 out Kante out in Hussen Semfuko, out Mutale in Kibu Dennis dk 79

Dakika ya 76 Namungo FC miss chance 

Dakika ya 71 Farid out in Rodgers Gabriel

Dakika ya 71 Abdallah Mfuko out in Buswita

Dakika ya 68 Mukwala out in Seleman Mwalimu

Dakika ya 68 Morice Abraham out in Ahoua

Dakika ya 66 Yakoub sace

Dakika ya 61 jezi namba 35 piga faulo, goal Rushine ndani ya 18

Rushine save dk 59

Dakika ya 57 Mukwala cheza faulo

Dakika ya 55 Abraham chezewa faulo 

Dakika ya 52 Namungo peleka mashambulizi Simba SC

Dakika ya 52 Maema of target 

Dakika ya 45 Mpanzu out in Maema, Kabunda out in Lupindo Charles 

Dakika 45 zimekamilika

 zimeongezwa dakika 2

Dakika ya 51 Rushine save

Dakika ya 49 Chamou save

Dakika ya 46 Mutalr long pasi

Dakika 45 Morice rusha

Kapombe chezewa faulo na Dilunga

Dakika ya 43 Chamou goal header asisti Mutale kwa pigo la kona nje ya 18 mguu wa kulia

Dakika ya 43 Mpanzu shot inaokolewa na kipa

Dakika ya 42 Mpanzu shot pasi

Dakika ya 41 Kapombe save

Dakika ya 39 Kapombe cheza faulo

Dakika ya 38 Mutale piga kona

Dakika ya 38 header gonga besela

Dakika ya 36 Mukwala on target

Dilunga piga kona ya kwanza katika mchezo

Read More

Friday, 26 September 2025

Simba SC 3-0 Fountain Gate, Uwanja wa Mkapa

08:47 0

 


Simba SC 3-0 Fountain Gate mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Septemba 25 2025 Uwanja wa Mkapa.

Mabao ya Simba SC yamefungwa na Rushine dakika ya 5, Ahoua dakika ya 36 na Sowah dakika ya 57.

Dk 90 namba nne off target 

Dk 89 Fadhil save on target Morice

Dk 89 Ahoua piga kona 

Dk 86 Nangu save 

Dk 83 Ahoua piga kona

Dk 82 Ahoua on target 

Dk Said on target 

Dk 79 otea dk 80

Dk 79 Chamou save

Dk 77 Sowah cheza faulo

Dk ya 75 Said Ramadhan piga kona 

Dk 71 Rushine out in Nangu, out Shomari Kapombe in Duchu

Dk 70 Mpanzh save

Dk 69 Fadhil Kisunga anzisha mashambulizi

Dk 69 Kapombe krosi 

Dk 68 Maema piga faulo

Dk 67 Kapombe rusha

Dk 67 Kante cheza faulo

Dk 65 Kagoma out in Maema

Dk 63 Ahoua piga kona 

Dk 63 Mpanzu chezewa faulo ndani ya 18 

Dk 62 Naby Camara  

Dk 60 out Hassan Ally in Anack Mtambi

Kapombe cheza faulo dk 58

Dk 57 Mpanzu asisti, goal Sowah

Dk 57 Ahoua piga kona

Dk 56 Kagoma of target 

Dk 54 Sowah of target 

Dk 54 Chamou save

Dk 53 Mpanzu krosi

Dk 52 Chamou piga faulo

Dk 50 Camara Naby rusha

Dk 49 Sowah of target 

Dakika ya 48 Mpanzu krosi

Dk 45 Morice in out Kibu

Dk 45 Mzamiru out in Kante

Zimeongezwa 2

Dk Sadik Ramadhani piga kona kwa Fountain Gate 

Dk 44 Elie Mokono of target 

Dk 41 Camara save

Dk 40 krosi Mpanzu

Dk 39 Kagoma save 

Dk 36 Ahoua goal kulia ndani ya 18 asisti Kagoma 

Dk 35 krosi Kapombe

Dk 34 Ahoua piga faulo

Dakika 33 Kagoma shot pasi

Dk 25 Kulandana of target 

Dk 24 Jean piga faulo

Dk 23 Lamela piga faulo

Dk 22 Mpanzu dribe

Dk 22 Mzamiru pasi

Dk Elie Mkono dribe 

Dk 19 Mzamiru pasi

Dk 18 Fadhilu save

Dk 18 Ahoua piga faulo

Dk 17 Mpanzu chezewa faulo

Dk 16 Rushine krosi

Dk 15 save Kagoma

Dk 14 Mzamiru pasi

Dk 14 Rushine save

Dk 13 Lamela rusha

Dk 13 Kibu poteza pasi ndani ya 18

Dk 12 Lamela rusha

Dk 10 Ahoua poteza pasi

Dk 8 Kagoma chezewa faulo

Dk 8 Chamou save 

Dk 7 Daniel piga faulo

Dk 6 Sowah cheza faulo

Dk 5 Rushine goal header

Dk 5 Ahoua piga kona

Dk 4 Fadhil Kisunga save 

Dk 4 Rushine krosi

Dk 3 Kapombe rusha

Dk 3 Rushine touch

Dk 2 Daniel Jolam save

Dk 2 Elie Mokono of target 

Kapombe rusha dk 1

Sowa krosi dk 1

Read More

Post Top Ad