Dizo Click

Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Post Top Ad

Saturday, 9 August 2025

WAPINZANI WA AZAM FC, SINGIDA BLACK STARS KIMATAIFA

18:08 0

 


Tanzania ina timu tatu kwenye anga la kimataifa katika Kombe la Shirikisho Afrika msimu wa 2025/26.

Klabu ya Azam FC ya Tanzania imepangwa kucheza na El Merriekh Bentiu ya Sudan Kusini kwenye hatua za awali michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

KMKM ikipangwa kucheza dhidi ya AS Port ya Djibouti. Azam FC msimu wa 2024/25 ilikuwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu itakuwa katika Kombe la Shirikisho Afrika.

Kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) ambapo Tanzania inawakilishwa na klabu tatu jumla. Klabu mbili kutoka Tanzania bara na moja kutoka Zanzibar.

Singida Black Stars ya Tanzania kwenye anga la kimatafa itaanzia ugenini ambapo kwenye mchezo wa awali wa Kombe la Shirikisho Afrika.

Ni Rayon Sports ya Rwanda kwenye anga la kimataifa imepangwa kucheza na Singida Black Stars ambapo ni Singida Black Stars watakuwa ugenini.

Agosti 9 2025 droo imechezwa katika studio za Azam TV, Dar ikiwa ni hatua za awali kwenye anga la kimataifa msimu mpya wa 2025/26.

 

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.

Read More

Friday, 11 July 2025

BEKI MPYA SINGIDA BLACK STARS AFUNGUKA

17:15 0


NYOTA Kelvin Kijili ambaye ni ingizo jipya ndani ya Singida Black Stars akitokea kikosi cha Simba SC ameweka wazi kuwa yupo tayari kwa ajili ya kupambana kutimiza majukumu kwenye timu hiyo kitaifa na kimataifa.

Kijili ametambulishwa rasmi ndani ya Singida Black Stars Julai 10 2025 ikiwa ni mchezaji wa kwanza kutambulishwa ndani ya Singida Black Stars.

Msimu wa 2024/25 alikuwa ndani ya kikosi cha Simba SC. Kwenye kikosi cha Simba SC hakuwa na nafasi kikosi cha kwanza hakufikisha mechi 15 za ligi kati ya 30 ambazo timu hiyo ilicheza.

Anajiunga na Singida Black Stars ambayo itashiriki Kombe la Shirikisho Afrika chini ya Kocha Mkuu, Miguel Gamondi ambaye aliwahi kuifundisha Yanga SC.

Kijili amesema: "Nimefurahi kusaini mkataba ndani ya Singida Black Stars nina amini kwamba nitafanya kazi kubwa kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu kitaifa na kimataifa."

Ni miaka miwili amesaini mchezaji huyo kwa ajili ya changamoto mpya msimu wa 2025/26 amerejea nyumbani kwa mara nyingine tena.

 

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.

Read More

CLATOUS CHAMA KWENYE RADA ZA ZESCO UNITED

16:48 0


 KIUNGO mshambuliaji wa Yanga SC, Clatous Chama anatajwa kuwa kwenye rada za Klabu ya Zesco United ya Zambia.

Chama ambaye alitambulishwa rasmi Yanga SC Julai Mosi 2024, mkataba wake wa mwaka mmoja umeggota mwisho.

Alitambulishwa hapo akiwa mchezaji huru akitokea kikosi cha Simba SC ambacho kimegotea nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

Taarifa zinaeleza kuwa mazungumzo ya wakala wa Chama na Zesco United yamefikia kwenye hatua nzuri kilichobaki nyota huyo kusaini na kutambulishwa ikiwa mabosi wa Yanga SC watamchunia moja kwa moja.

Yanga SC wanatambua mkataba wa mchezaji huyo umeisha na hawajafanya mazungumzo yoyote jambo linaloashiria kwamba ni asilimia kubwa hatakuwa kwenye ligi namba nne kwa ubora Afrika Clatous Chama msimu wa 2025/26.

Msimu wa 2024/25, Chama alifunga mabao sita na katika mabao hayo mabao mawili alifunga kwa mapigo huru akiwa nje ya 18.


Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.


Read More

Sunday, 20 April 2025

FOUNTAIN GATE WAZITAKA POINTI TATU ZA YANGA

18:51 0

 


WAPINZANI wa Yanga ndani ya Ligi Kuu Bara kuelekea kwenye mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa Aprili 21 2025 Uwanja wa Tanzanite, Kwaraa Fountain Gate wamebainisha kuwa wamepata mbinu za wapinzani wao hivyo wanajua namna watakavyofanya kazi kuwadhibiti.

Yanga ni vinara ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mechi 25 ni pointi 67 wamekusanya kibindoni na safu ya ushambuliaji imetupia jumla ya mabao 64 ikiwa ni safu kali kwenye kumalizia nafasi ambazo zinatengenezwa ndani ya uwanja kwenye ligi.

Inakutana na Fountain Gate ambayo namba mbili kwa timu ambazo zimeruhusu mabao mengi ndani ya ligi ambayo ni 47 baada yakucheza mechi 26 ikiwa nafasi ya 9 na pointi zake kibindoni ni 29.

Issa Mbuzi amesema kuwa wanatambua ubora wa Yanga ulipo na udhaifu kwa kuwa waliwatazama kwa ukaribu kwenye mchezo dhidi ya Stand United uliochezwa Uwanja wa KMC, Complex, Aprili 15 2025 na ubao ukasoma Yanga 8-1 Stand United.

“Tunawatambua vizuri hawa Yanga na kwenye mchezo wao dhidi ya Stand tulikuwa na wataalamu wakusoma mbinu zaidi ya wanne, wameniambia wameona namna itakayotupa matokeo kwenye mchezo wetu Aprili 21 tukiwa nyumbani.

“Eneo la kiungo kuna matatizo pale na wanaye Aziz Ki ambaye huyu tutampa mtu wakutembea naye hatua kwa hatua ndani ya uwanja, utakuwa mchezo mgumu lakini tunahitaji pointi tatu zao ili tujihakikishie nafasi ya sita kwenye msimamo.”


Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu usipange kukosa.


Read More

Sunday, 2 June 2024

SIMBA KUJIPANGA UPYA TENA

16:09 0


 
UONGOZI wa Simba umeweka wazi kuwa utafanyia kazi makosa ambayo yamepita ili kurejea kwenye ubora wao kwa kuwa nyakati ambazo wamepita zimewaumiza.

Ipo wazi kuwa Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Juma Mgunda imegotea nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 69.

Kwenye mchezo wa funga msimu 2023/24 ilikuwa ni dhidi ya Geita Gold waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 watupiaji wakiwa ni Saido Ntibanzokiza na Willy Onana.

Imepishana na taji la ligi pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika na inakwenda kushuhudia bingwa mpya wa CRDB Federation Cup akipatikana leo kati ya Azam FC na Yanga, fainali inayotarajiwa kuchezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba ameweka wazi kuwa nyakati ambazo wamepitia ni ngumu na hazijawafurahisha hivyo wanapambana kurejea kwenye ubora.

“Hatujapenda na tumekuwa na huzuni kwa kuwa tumepoteza kila kitu ambacho tulikuwa tunakipigania kwenye msimu ulioisha.

“Yote kwa yote yaliyopita tunayachukua na tunakwenda kuyafanyia kazi kwa ajili ya kuwa bora wakati ujao mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi.”

Read More

Tuesday, 2 April 2024

JESHI LA YANGA LITAKALOIBUKA KWA MADIBA HILI HAPA

11:12 0

 


MSAFARA wa kikosi cha Yanga umekwea pipa mapema Aprili 2 2024 kuwafuata wapinzani wao Mamelodi Sundowns kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa unaotarajiwa kuchezwa Aprili 5 siku ya Ijumaa.

Ni mchezo wa hatua ya robo fainali ikiwa ni mkondo wa pili baada ya ule uliochezwa Machi 30 ubao wa Uwanja wa Mkapa kusoma Yanga 0-0 Mamelodi Sundowns.

Hiki hapa kikosi cha Yanga chenye wachezaji 26 namna hii:-

Djigui Diarra,
 Aboutwalib Mshery na  Metacha Mnata kwa upande wa makipa ambapo chaguo la kwanza ni Diarra
 Bakari Mwamnyeto, Ibrahim Bacca,  Dickson Job, Yao Attohoula, Nickson Kibabage, Joyce Lomalisa, Gift Fred na Kibwana Shomari upande wa mabeki.

Viungo wa ukabaji ni  Khalid Aucho, Zawadi Mauya, Salum Abubakar, (Sure Boy), Jonas Mkude, Mudathir Yahya na Maxi Nzengeli

Viungo washambuliaji kuna Pacome Zouzoua, Aziz Ki, Augustine Okrah, Skudu Makudubela, Farid Mussa
na Denis Nkane.


Washambuliaji ni Clement Mzize,  Joseph Guede na Kennedy Musonda ambapo kwenye mchezo wa Uwanja wa Mkapa wote walipata nafasi ya kuchez.

Read More

Wednesday, 27 March 2024

MNYAMA AMVUTIA KASI MWARABU KWA MKAPA KIMATAIFA

13:01 0

 


KIKOSI cha Simba kimerejea Dar baada ya kuweka kambi Zanzibar kwa muda ikiwa ni maandalizi ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa.

Ni Machi 29 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa ambapo kwa sasa hamasa zinaendelea mtaa kwa mtaa kuwahamasisha mashabiki wa Simba kujitokeza Uwanja wa Mkapa kushuhudia mchezo huo.

Ahmed Ally, Meneje wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba amesema kuwa Ijumaa kazi ni moja kwa mashabiki kujitokeza uwanjani kushangilia mwanzo mwisho katika mchezo huo na malengo ni kuona wanapata ushindi ndani ya dakika 90.

 

 

KOCHA APEWA MAJUKUMU MAZITO

Ally amesema kuwa uzoefu alionao kocha wa timu hiyo ni moja ya sababu itakayoongeza nguvu kwa timu hiyo kuvuka hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika na kutinga hatua ya nusu fainali.

Ikumbukwe kwamba Simba hesabu kubwa kwa msimu huu ni kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kugotea mara kwa mara hatua ya robo fainali jambo ambalo limewafanya viongozi wa timu hiyo kubainisha kwamba inatosha.

"Kwa uzoefu na ubora wa kocha Abdelhak Benchikha tunaamini atatuvuzusha kwenda Nusu Fainali.

Tunaamini kwamba kila kitu kinawezekana na hilo linatupa nguvu kwa ajili ya kuwa kwenye ushindani mkubwa ambao upo ndani ya uwanja kwa kuwa kila kitu kinawezekana na muda ni sasa.

 “Hakuna katika dunia hii mtu yoyote wakuwazuia mashabiki wa Simba wanapotaka jambo lao, tuungane tupige goti tufanye kila linalowezekana ili tutimize malengo yetu.

“Wachezaji ni wasikivu na wanatambua kazi kubwa inahitajika kufanyika uwanjani hivyo muda ni sasa kuwa kwenye mpango kazi wa kutafuta ushindi ndani ya uwanja, mashabiki tujitokeze kwa wingi kwani kila mchezaji anapenda kuona furaha inabaki ndani ya Simba.

ULINZI KUONGEZEWA DOZI

Benchi la ufundi la Simba limebainisha kuwa makosa ambayo yamekuwa yakifanyika kwenye mechi za ligi yanafanyiwa kazi kwa umakini ili kuwa na safu imara ya ulinzi kwenye mechi zao wanazocheza kutokana na ushindani kuwa mkubwa kitaifa na kimataifa.

Kwenye safu ya ulinzi ni Henock Inonga, Che Malone, Mohmaed Hussein, Shomari Kapombe ni miongoni mwa wachezaji wanaounda safu ya ulinzi ya timu hiyo ya Simba ambayo ina kazi kupambana dhidi ya Al Ahly.

Ipo wazi kwamba ndani ya Ligi Kuu Bara, safu ya ulinzi ya Simba haijawa kwenye mwendo bora katika mechi zake tofauti na zile inazocheza kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Seleman Matola, kocha msaidizi wa Simba amesema kuwa wanatambua makosa yalipo jambo linalowafanya wafanye kazi kwa umakini kuelekea kwenye mechi zijazo kwa kuwaongezea wachezaji wao dozi nyingine.

“Unaona kwenye mechi ambazo tunacheza tunapata ushindi na wakati mwingine tunawapa ruhusa wapinzani kutufunga huwa tunaongea na wachezaji na tutaongeza dozi nyingine kwenye uwanja wa mazoezi.

“Kikubwa ni kuwa makini kwa kuwa mchezo wa mpira ni mchezo wa makosa, kuelekea kwenye mechi zetu zijazo tuna imani tutakuwa imara hilo linawezekana kutokana na wachezaji kujituma na kutimiza majukumu yao kwa ushirikiano,”.

Kikosi cha Simba baada ya kucheza mechi 19 ndani ya ligi ni mabao 18 ukuta umeruhusu ikiwa namba moja kwa timu ambazo zimefungwa mabao mengi ndani ya tatu bora msimu wa 2023/24.

AL AHLY NDANI YA DAR

Kete inayofuata kwa Simba ni Machi 30 2024 itakuwa dhidi ya Al Ahly ambao tayari Machi 27 wameanza mapema safari kwa ajili ya kuwasili Dar kufanya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo.

Mchezo ujao kwa Simba ni wa Ligi ya Mabingwa Afrika itakuwa dhidi ya Al Ahly unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Machi 29 tayari wapinzani wao wameanza safari kuja Dar wanatarajiwa kuwasili Machi 27 kufanya maandalizi ya mwisho kuelekea katika mchezo huo.

Kila timu inautazama mchezo huo kwa hesabu kubwa za kupata ushindi kutokana na ukubwa wa mashindano hayo barani Afrika.

 

Read More

Post Top Ad